Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na sala na amani zimshukie Mtume wa Mwenyezi Mungu, familia yake na maswahaba zake.
Ama siku utakayosafiri kabla ya jua kuzama, lazima kwanza ufunge. Kwa sababu utakuwa mkaazi mwanzoni mwake, basi ukisafiri ndani yake unatakiwa utimize saumu yako na usiifungue kwa kuzingatia kauli ya mafaqihi wanaomkataza mfungaji kufuturu ikiwa amesafiri mchana. Tazama Fatwa No.: 128994 kuhusu madhehebu ya mafaqihi kuhusiana na msafiri anayefungua saumu baada ya kuanza kufunga.
Hakuna kosa juu yako kwa kufuturu wakati wa safari yako baada ya kuanza safari yako. Kwa sababu Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: “Lakini atakayekuwa mgonjwa miongoni mwenu au yumo safarini, basi ijumuishwe idadi (ya siku) katika siku nyengine.[Surat Al-Baqarah: 184]
Ukifika katika nchi yako, Libya, lazima ufunge kwa sababu safari yako imekatizwa Tazama Fatwa No. 375982.
Na Mungu anajua zaidi.